Wataalamu wetu wa kitiba

Wafahamu baadhi ya madaktari, wanasayansi, na wastadi wa kitiba wanaofanya kazi Ada.

Wataalamu wetu wa ndani hutoa ufahamu wa kitiba na usimamizi katika maeneo mbalimbali ya usitawishaji wa bidhaa, utafiti, na maudhui ya kitiba ya intaneti 

Uongozi wa Masuala ya Kitiba

Claire Novorol

Mwanzilishi-mwenza & Afisa Mkuu wa Masuala ya Kitiba

Dk. Claire Novorol

Mwanzilishi-mwenza & Afisa Mkuu wa Masuala ya Kitiba

Dk. Claire Novorol

Claire ni daktari. Alifanya kazi kama daktari wa watoto jijini London kabla ya kubobea katika jenetikia. Amehitimu Shahada mbili, yaani ya Patholojia na ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Bristol, na Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Sayansi ya Mfumo wa Neva kutoka Chuo Kikuu cha Cambridge, nchini Uingereza. Claire anasimamia ubora wa kitiba pamoja na timu zetu za kitiba. Anawakilisha sauti za wagonjwa na wataalamu wa huduma za afya ili kuhakikisha bidhaa zetu zinakidhi mahitaji yao.

Martin Hirsch

Mwanzilishi-mwenza & Mshauri Mkuu wa Masuala ya Kisayansi

Prof. Dk. Martin Hirsch

Mwanzilishi-mwenza & Mshauri Mkuu wa Masuala ya Kisayansi

Prof. Dk. Martin Hirsch

Martin ana Shahada ya Uzamivu katika Sayansi ya Mfumo wa Neva na diploma katika Fiziolojia. Martin ni mtafiti wa masuala ya kitiba aliyegeuka kuwa mjasiriamali, na alihama kutoka nadharia hadi uvumbuzi baada ya kuchapisha kazi yake kuhusu miundo mfano ya neva (nerve modeling) katika Jarida la Kisayansi la Nature. Ubia wake wa kwanza ulikuwa kwenye mpango wa uundaji wa neva ambao uliokoa maelfu ya wanyama kutoka kwenye jaribio la maabara. Alitengeneza toleo la kwanza la Ada kwa ajili ya madaktari na anaendelea kutoa mwelekeo wa namna Ada inavyojifunza leo. Martin ni mjukuu wa Werner Heisenberg, ambaye ni mshindi wa tuzo ya Nobeli.

Utawala wa Masuala ya Kitiba

Ewelina Türk

Ewelina Türk

SVP, Bidhaa ya Kitiba

Ewelina anaongoza timu yetu ya maarifa ya kitiba. Amezaliwa Poland na kukulia Ujerumani. Ewe amesomea udaktari katika chuo cha tiba cha Charité, Berlin, akiweka maslahi zaidi kwenye magonjwa ya watoto, haswa huduma za dharura na kinga. Zaidi ya hayo, Ewelina hivi sasa anamalizia Shahada ya Uzamivu katika magonjwa ya baridi yabisi kwa watoto.

Tauseef Mehrali

Tauseef Mehrali

VP of Medical Safety and Regulatory Affairs

Tauseef ni daktari wa Huduma ya Afya ya Kitaifa ya Uingereza (NHS). Alihitimu Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Tiba, Maadili na Sheria katika Chuo Kikuu cha Cambridge. Alipata Shahada yake ya kwanza ya Udaktari na Upasuaji kwa ufaulu mkubwa (distinction) kutoka Chuo Kikuu cha Birmingham. Tauseef ni mwanachama wa Royal College of Pediatrics & Child Health na Royal College ya Madaktari (GPs). Maeneo yake ya utafiti ni pamoja na utafutaji wa ufumbuzi wa masuala magumu, kuboresha matokeo ya mtumiaji na uzoefu wa wataalamu wa afya, na elimu ya tiba.

Shubhanan Upahyay

Dk. Shubhanan Upadhyay

Mkurugenzi wa Ubora wa Kitiba

Dk. Upadhyay ni mmoja wa madaktari wa dharura wa mpango wa Huduma za Afya ya Taifa - NHS (Uingereza) na mshiriki wa mpango wa Wajasiriamali wa Masuala ya Kitiba (2018/19). Ana Shahada ya Udaktari na Shahada ya Upasuaji kutoka Chuo cha Imperial. Maeneo aliyo na utaalamu nayo ni pamoja na masuala ya afya duniani, tiba ya kitropiki, na elimu ya Kitiba. Kikazi anafahamika zaidi kama “Dk. Shubs” na huandika kuhusu masuala ya afya duniani, tiba ya kitropiki, elimu ya kitiba, na uwezo wa teknolojia kusaidia huduma ya mgonjwa na usimamizi thabiti wa afya.  

Adel Baluch

Dk. Adel Baluch

Mkurugenzi wa Masuala ya Kitiba

Dk. Baluch anafanya kazi kama daktari chini ya Mpango wa Huduma za Afya ya Taifa - NHS (Uingereza). Ni mhitimu wa Bartholomew’s na Chuo cha Udaktari cha Royal London, na ana Shahada ya Udaktari na Shahada ya Upasuaji kutoka Chuo Kikuu cha Queen Mary cha London. Adel pia ana sifa za uzamili baada ya kufaulu mitihani yake na kufuzu uwanachama wa Chuo cha Madaktari cha Royal (Royal College of Physicians), Chuo cha Royal cha Madaktari wa Magonjwa ya Jumla (General Practitioners), na Bodi ya Marekani ya Tiba ya Mtindo wa Maisha (American Board of Lifestyle Medicine).

Bidhaa ya Kitiba

Kirsten Gray

Dk. Kirsten Gray

Kiongozi wa Bidhaa ya Kitiba, Jukwaa la Kitiba

Dk. Gray alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Otago nchini New Zealand, na wakati huo alishiriki pia katika miradi ya utafiti katika maeneo ya magonjwa ya akili. Baada ya kuhitimu, alifanya kazi kama daktari hospitalini kwa miaka kadhaa, akiweka masilahi katika magonjwa ya akili na watoto. Kabla ya kujiunga Ada, Kirsten alifanya kazi katika Hospitali ya Watoto ya Starship huko Auckland (New Zealand). 

Alicia Mehl

Alicia Mehl

Kiongozi wa Bidhaa ya Kitiba, Data

Alicia alipata mafunzo ya udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza kule London School of Hygiene & Tropical Medicine na ni Mtaalamu wa Magonjwa ya Mlipuko katika timu yetu ya Magonjwa ya Mlipuko & Afya ya Jamii. Ana uzoefu wa maeneo mbalimbali akifanya kazi katika nchi zenye rasilimali chache, ikiwemo Msumbiji, Nigeria, na Saint Lucia. Alicia anapendelea kuunganisha nguvu ya Akili Bandia (AI) na mbinu za kukabiliana na magonjwa ya milipuko ili kufanikisha kufikia matokeo bora zaidi ya afya kwa wote.  

Malek Hamzeh

Dk. Malek Hamzeh

Meneja Mwandamizi wa Usalama wa Kitiba

Dk. Hamzeh alipata msaada wa masomo ili kusomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Istanbul, Uturuki, na kuhitimu Shahada ya Udaktari. Alifanya kazi kama daktari wa familia kwenye kituo cha afya ya jamii Istanbul, ambapo kwa kiasi kikubwa wagonjwa walikuwa ni wakimbizi walioshindwa kupata huduma za afya hapo awali. Anaamini upatikanaji wa huduma za afya ni haki ya kila mtu, na anafurahi kujiunga na Ada ili kuwezesha upatikanaji huo.

Nico Meißner-Bendzko

Nico Meißner-Bendzko

Kiongozi wa Timu, Maarifa ya Kitiba

Nico alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka Chuo cha Charité, Berlin. Alianza kufanya kazi Ada mwaka 2015 wakati akiwa bado mwanafunzi, akiongozwa na shauku yake ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya ukosefu wa usawa katika huduma za afya. Maeneo ya kitiba aliyojikita ni pamoja na elimu ya neva (neurology) na tiba za dharura. Hivi sasa anakamilisha tasnifu yake ya udaktari katika kitengo cha kiharusi cha Chuo Kikuu cha Charité.

Dk. Angela Beling

Dk. Angela Beling

Kiongozi wa Timu, Maarifa ya Kitiba

Angela alisomea Udaktari katika Universidad Nacional de Cuyo nchini Argentina ambako alijikita katika masuala ya magonjwa ya akili. Baada ya miaka michache ya kazi hospitalini, alianza kusomea Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Afya ya Binadamu (Health Humanities). Mnamo mwaka 2017, baada ya kuhitimu PhD yake, Angela alijiunga na Ada. Maeneo yake makuu ya utafiti ni kwenye masuala ya afya ya jamii, elimu-maadili ya utafiti wa kitiba na kibiolojia (bioethics), na afya ya akili, hasa kwenye afya ya uzazi na afya ya akili ya mama wakati wa uzazi.

Johannes Scholz

Dk. Johannes Scholz

Kiongozi wa Timu, Maarifa ya Kitiba

Johannes alisomea udaktari katika mji wa Vienna, nchini Austria. Baada ya kuhitimu masomo yake, alifanya kazi kwa miaka minne katika idara za rediolojia (radiology) na redionkolojia (radiooncology) katika mji wa Berlin, nchini Ujerumani. Maeneo yake makuu ya utafiti yanahusiana na onkolojia, neurolojia, na tiba ya kidigitali.  

Merret Eiling

Merret Eiling

Msimamizi wa Bidhaa za Kiufundi katika Maarifa ya Kitiba

Merret alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka Chuo cha Charité, Berlin. Alianza kufanya kazi Ada mwaka 2014, na kupata uzoefu mkubwa wa kitaalamu katika afya ya kidijitali na kutoa mwelekeo wa namna tunavyounda maarifa ya kitiba. Merret anapenda masuala ya afya ya kidijitali na uwezekano wake katika kusaidia mifumo ya afya duniani kote.

Chi-Yu Liu

Dk. Chi-Yu Liu

Mtaalamu wa Ubora wa Kitiba

Dk. Liu alifanya kazi kama daktari mashariki mwa Taiwani. Shauku yake ya kusimamia haki na ustawi wa watoto, haswa katika afya, ilimfanya asomee Shahada ya Uzamili katika masuala ya Haki za Watoto huko Potsdam, Ujerumani.

Nils Metzger

Nils Metzger

Mhandisi wa Bidhaa ya Kitiba

Nils amehitimu Shahada ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Rheinische Friedrich-Whilhelms,  Bonn. Akiwa kama mwanafunzi msaidizi, alihudumu kwenye Kitengo cha Wagonjwa Mahututi (ICU) na wodi ya kawaida ya Kliniki ya Chuo Kikuu cha Bonn na kumaliza mafunzo yake kwa vitendo (internship) Berlin ambapo alijikita kwenye taaluma ya magonjwa ya watu wazima na taaluma ya magonjwa ya mfumo wa mkojo. Wakati wa masomo yake, Nils alitoa mchango katika uundaji wa hifadhidata ya watu wenye kifafa kinachotokana na inflamesheni kwenye ubongo (limbic encephalitis). Nils ana shauku ya kusaidia kuboresha maisha ya watu duniani kote kupitia teknolojia ya Ada.

Michal Stebnicki

Dk. Michal Stebnicki

Mhandisi Mwandamizi wa Maarifa ya Kitiba

Dk. Stebnicki alisomea udaktari jijini Lodz na Wroclaw kabla ya kuhitimu Shahada yake ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Wroclaw Kitivo cha Tiba. Michal amebobea kwenye magonjwa ya akili na katika eneo hilo, alipata uzoefu zaidi wa kikazi kama mkurufunzi na kama daktari msaidizi katika kliniki za Berlin.

Victor Hertz

Victor Hertz

Mhandisi Mwandamizi wa Maarifa ya Kitiba

Victor alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka Chuo cha Charité, Berlin. Alianza kazi Ada kama mwanafunzi mfanyakazi wakati wa masomo yake mwaka 2013. Victor pia alimaliza mafunzo ya miezi 2 katika Hospitali ya Kathmandu Model, nchini Nepal. Maeneo ya kitiba anayopendelea ni pamoja na rediolojia na taaluma ya magonjwa ya kitropiki.

Nisha Kini

Dk. Nisha Kini

Mhandisi wa Maarifa ya Kitiba

Nisha amehitimu Shahada zake za Udaktari na Upasuaji kutoka Chuo Kikuu Cha Maharashtra Cha Sayansi ya Afya. Pia alihitimu Shahada yake ya Uzamili ya Afya ya Jamii katika elimu ya magojwa ya mlipuko na takwimu za Kibiolojia kutoka Chuo Kikuu cha Massachusetts Amherst. Alifanya kazi kama afisa mkazi wa masuala ya kitiba nchini India, na halafu akafanya kazi kama mtafiti katika ulimwengu wa taaluma na sekta ya tiba katika Marekani na Ulaya. Nisha anapenda sana matumizi ya AI katika huduma za afya na uwezekano wa kusaidia mamilioni ya watu ulimwenguni kote kupitia matumizi hayo.

Carina Coltuneac

Dk. Carina Coltuneac

Mhandisi wa Maarifa ya Kitiba

Carina alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka Chuo cha Udaktari na Ufamasia "Gr. T. Popa" lasi. Baada ya kuhitimu, alipata uzoefu wa kazi (internship) ya masuala ya kitiba katika taaluma ya magonjwa ya figo (nephrology) katika Hospitali ya "C.I. Parhon" lasi, nchini Romania, na Hospitali ya CHR Orleans, Ufaransa.

Nicola D'Avino

Dk. Nicola D’Avino

Mhandisi wa Maarifa ya Kitiba

Nicola alipata Shahada ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Naples Federico II, nchini Italia. Baada ya kuhitimu, alitumia mwaka 1 nchini Uswizi na kupata uzoefu wa kazi katika idara za kadiolojia na dharura. Baada ya kurudi Italia, Nicola aliendelea kufanya kazi kama daktari kwa miaka 3 katika huduma ya msingi na ya dharura. Katika kipindi hicho, alipata pia utaalamu wa tiba ya magonjwa mbalimbali kwa watu wa rika tofauti.

Dk. Vedika Kundi

Dk. Vedika Kundi

Mhandisi wa Maarifa ya Kitiba

Vedika alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka chuo Kikuu cha Charles, nchini Prague. Alishika nyadhifa katika kliniki kadhaa nchini Uingereza na kufanya kazi mbalimbali za utaalamu wa kitiba na upasuaji. Hivi sasa anamalizia Shahada ya Uzamili kwenye masuala ya afya duniani katika Chuo Kikuu cha Charité, Berlin, akizingatia mchango unaoweza kuletwa na afya ya kidijitali kwenye mazingira ya nchi zenye kipato cha chini. Vedika anapenda masuala ya huduma za afya zinazozingatia utoaji wa kinga, elimu pana ya afya, na upunguzaji wa ukosefu wa usawa katika huduma za afya duniani.

Daniel Glauert

Daniel Glauert

Mhandisi wa Maarifa ya Kitiba

Daniel ni mtahiniwa wa udaktari katika Chuo cha Udaktari cha Charité, Berlin na mmoja wa wanafunzi wetu wa maarifa ya kitiba. Ana uzoefu katika Chama cha Kitaifa cha Wanafunzi wa Udaktari, bunge la Chuo Kikuu cha Humboldt, mafunzo ya udaktari kwa vitendo katika nchi zinazoendelea. Daniel anavutiwa na siasa za masuala ya afya na masuala ya afya ulimwenguni. Amejidhatiti kuleta mustakabali wa tiba katika mitaala ya chuo kikuu na anashirikiana kuendeleza na kufundisha vipindi kadhaa juu ya afya ya kidijitali. 

Utafiti

Milan Jovanovic

Milan Jovanovic

Mtafiti wa Kitiba Mwandamizi

Milan alipata Shahada yake ya Udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Kragujevac, nchini Serbia. Na baadaye alipata Shahada ya Uzamili katika Biolojia ya Seli na Molekuli kutoka Chuo Kikuu cha Coimbra, nchini Ureno, na Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Mishipa ya Fahamu katika Chuo Kikuu cha Charité, jijini Berlin.

Lee Stopak

Lee Stopak

Mwanabiolojia Mwandamizi wa Utafiti

Lee alihitimu mafunzo ya awali ya udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Maryland, akibobea katika Biolojia ya Mfumo wa Neva na Jenetikia kabla ya kumaliza Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Mfumo wa Neva katika Chuo cha Charité, Berlin. Ameshika nyadhifa kadhaa za utafiti wa jenetikia, pamoja na wadhifa alioshika katika Taasisi ya Sayansi ya Weizmann huko Israeli.