1. Ada
  2. Magonjwa
  3. Upungufu wa madini ya chuma

Upungufu wa madini ya chuma

Imeandikwa na Timu ya Ada ya Maarifa ya Kitiba

Imesasishwa tarehe

Upungufu wa madini ya chuma ni nini?

Upungufu wa damu kutokana na kupungua kwa madini ya chuma ni kati ya aina kuu za upungufu wa damu. Ni hali ambayo mwili unakuwa hauna madini ya chuma ya kutosha ili kutengeneza hemoglobini. Hemoglobini ni protini kwenye seli nyekundu za damu ambayo ni muhimu katika kusafirisha oksijeni kwenye tishu za mwili.

Upungufu wa damu kutokana na kupungua kwa madini ya chuma ni kati ya aina kuu za upungufu wa damu. Ni hali ambayo mwili unakuwa hauna madini ya chuma ya kutosha ili kutengeneza hemoglobini. Hemoglobini ni protini kwenye seli nyekundu za damu ambayo ni muhimu katika kusafirisha oksijeni kwenye tishu za mwili.

Hali hii hutokea zaidi kwa wanawake wenye umri wa kuzaa, ingawa inaweza kumathiri mtu mwenye umri wowote. Sababu za hali hii kutokea hujumuisha kutoka damu kwa muda mrefu, magonjwa sugu ya mfumo wa kumeng'enya chakula. Kula lishe yenye kiwango kidogo cha vyakula vyenye madini ya chuma pia huweza kuwa chanzo ya hali hii kutokea.

Dalili za kawaida za upungufu wa damu ni uchovu, udhaifu, kukosa nguvu na kuishiwa pumzi. Wale walioathirika pia huweza kuwa na ngozi iliyopauka na matatizo ya nywele na kucha. Matibabu kawaida hujumuisha virutubisho vya madini ya chuma na kuongeza madini ya chuma kwenye lishe.

Watu wengi hupona vizuri kwa kutumia virutubisho na kwa kutibu chanzo ya hali hii kutokea.

Vihatarishi vya upungufu wa madini ya chuma

Upungufu wa damu humaanisha kuwa mwili hauna hemoglobini ya kutosha ili kusafirisha oksijeni mwilini. Madini ya chuma ni muhimu katika uzalishaji wa hemoglobini kwenye seli nyekundu za damu. Upungufu wa damu kutokana na upungufu wa madini ya chuma hutokea ikiwa mwili hauna madini ya chuma ya kutosha ili kutengeneza hemoglobini.

Mara nyingi hii hutokea mtu akipoteza kiwango kikubwa cha damu au wakati wa ujauzito. Mwili unahitaji kiwango kikubwa zaidi cha madini ya chuma katika kipindi cha ujauzito. Hali hii inaweza kutokea baada ya muda ikiwa mtu hawezi au hapati madini ya chuma ya kutosha kwenye lishe. Upungufu wa madini ya chuma ni kati ya visababishi vikuu vya upungufu wa damu. Hali hii hutokea zaidi kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa.

Dalili za upungufu wa madini ya chuma mwilini

Watu wenye upungufu wa damu kiasi mara nyingi hawana dalili. Dalili za kawaida ni pamoja na:

  • Uchovu
  • Udhaifu
  • Matatizo ya kupumua
  • Kupauka kwa ngozi

Dalili zingine zinaweza kujumuisha:

  • Matatizo ya uzingativu
  • Maumivu ya kichwa
  • Kucha zinazovunjika kirahisi
  • Upotevu wa nywele
  • Kingo za kinywa kupasuka
  • Ugumu wa kumeza
  • Ulimi kuuma

Utambuzi

Utambuzi hufanywa kulingana na dalili na historia ya matibabu. Vipimo vya damu hufanywa ili kuchunguza viwango vya hemoglobini pamoja na idadi na ukubwa wa seli nyekundu za damu. Viwango vya madini ya chuma pia hupimwa. Vipimo vingine huweza kuhitajika ili kutambua chanzo cha upungufu wa madini. Kipimo cha endoscopy, ambapo kamera hupitishwa mdomoni ili kuangalia mfumo wa umeng'enyaji chakula, huweza kufanywa kwa ajili ya utambuzi.

Matibabu

Ikiwa upungufu wa madini ya chuma husababishwa na ugonjwa mwingine, basi ugonjwa huu unapaswa kutibiwa. Hii huweza kuzuia upungufu zaidi wa madini ya chuma au matatizo katika ufyonzaji wa madini haya.

Ikiwa mtu aliyeathirika hana matatizo yoyote ya ufyonzaji wa madini ya chuma, wanapaswa kula vyakula vyenye madini ya chuma. Dengu, wali wa kahawia na maharage hupendekezwa zaidi. Mboga za majani na matunda yaliyokaushwa kama vile aprikoti na mizambarau pia husaidia. Samaki, nyama na mayai pia vina viwango vikubwa ya madini ya chuma. Watu wenye uwekezaji mdogo mwilini wa madini ya chuma huweza kutumia virutubisho.

Ikiwa viwango vya madini ni chini sana na mtu anahitaji viwango vikubwa ya madini ya chuma, basi madini haya huweza kuongezwa mwilini kupitia mishipa ya damu.

Kinga

Lishe yenye manufaa kiafya huweza kuzuia hali hii. Kula vyakula vya kutosha vyenye madini ya chuma ni muhimu. Kwa kuwa wanawake wajawazito wapo kwenye hatari zaidi ya kupata upungufu wa damu, wanapaswa kuzingatia kutumia virutubisho.

Ubashiri

Matokeo ya hali hii kwa kawaida ni mazuri. Watu wengi huweza kutibu na kumudu upungufu wa damu kwa kutumia virutubisho. Hii ni kweli haswa ikiwa upungufu wa madini ya chuma hausababishwi na ugonjwa mwingine. Hata visa hivi, uponaji hutegemea chanzo cha hali hii kutokea.


Washirikishe wengine kwenye makala hii: